Friday, April 17, 2009

SANDUKU LA AGANO LIKO WAPI?


Huu ni mfano wa sanduku la agano ambalo wana wa Israel waliambiwa watengeneze na Mussa wakiwa nyikani wakitoka Egypt (Misri) wakielekea promised land (Nchi ya ahadi). Sanduku hilo lilikuwa ni kama box la mbao lililotengenezwa na aina moja ya mbao inayoitwa (acacia wood) iliyofunikwa na dhahabu. Lilikuwa la urefu wa 1.15 metres, upana wa 0.7 metres na kimo cha 0.7 metres. Ilikuwa inabebwa na mishikio miwili mirefu ambayo ilikuwa imetengenezwa kwa mbao hiyo ya acasia ambazo pia zilikuwa zimefunikwa na dhahabu. Juu ya sanduku kuliwekwa makerubi wawili waliokuwa wamegeukiana mabawa yao yakiwa yamegusana. Uwepo wa Mungu haukuwepo ndani ya sanduku bali ulikuwa juu yake katikati ya hao makerubi. Uwepo wa Mungu juu ya sanduku hilo ulikuwa kama nuru. Kuhani mkuu alipaswa kufunika macho asiione nuru hiyo ("hakuna mwanadamu anionaye na akaishi" Kutoka 33 : 20) kila alipokuwa akiingia lilipokuwa sanduku ambapo ni patakatifu pa patakatifu. Hapa ndipo ambapo Mungu alipokuwa akiionana na Musa. Sanduku hili lilikuwa likibebwa na wana wa Walawi pekeyake hakuna mwingine aliyeruhusiwa kulishika, yeyote aliyedhubutu kulishika pasiporuhusiwa alikufa papohapo. Hao makerubi wawili wanawakilisha utukufu wa Mungu. Ndani ya sanduku hili kulikuwa na:


  1. Mawe mawili yaliyokuwa yameandikwa amri kumi za Mungu

  2. Fimbo ya Aron iliyoota mauwa

  3. Chombo cha dhahabu kilichokuwa na manna waliyokula wana wa Israel nyikani


Sanduku hilo lilikuwa linakaa patakatifu pa patakatifu, chumba cha ndani kabisa katika hema la kukutania. Aliyekuwa anaruhusiwa kuingia mahala hapo lilipokuwa sanduku hilo ni kuhani mkuu na alikuwa anaruhusiwa kuingia mara moja kwa mwaka. Kabla ya Kuhani mkuu kuingia patakatifu pa patakatifu alikuwa ni lazima aingie na damu ya mwana kondoo kwa niaba ya dhambi zake yeye mwenyewe na dhambi za wana wa Israel.


Sanduku la agano lilikuwa ndani ya hekalu lililojengwa na Solomon mpaka hekalu hilo lilipokujwa kuvunjwa mikononi mwa utawala wa Babylon ukioongozwa na Nebuchadnezzar. Kilichotokea kwa sanduku hilo hakijulikani ingawa haiwezekani kuwa lilichukuliwa na majeshi ya Babylon kama vilivyochukuliwa vyombo vingine vya hekalu kwasababu katika list ya vitu walivyovichukua sanduku la agano halikutajwa. Kulingana na baadhi ya vyanzo vya habari inasemekana kuwa mfalme Josiah, mmojawapo wa wafalme wa mwisho kutawala enzi za hekalu la kwanza, kutokana na unabii uliokuwa umetolewa alijua kuwa Jerusalem itavamiwa na Babylon, akalificha sanduku la agano. Alipolificha sanduku imekuwa kitendawili. Chanzo kingine cha habari kinasema kuwa mfalme Solomon alionyeshwa kuwa Hekalu litakujwa kuvunjwa na majeshi ya Babylon, kwahiyo akaandaa pango karibu na bahari ya shamu (dead sea) ambapo Josiah akaja kulificha sanduku. Na pia inasemekana nabii Yeremia (Jeremiah) alilificha sanduku chini ya Hekalu lililojengwa na Solomon. Na hata kuna tetesi ya kuwa hapa Tanzania kwenye misitu ya monduli kuna chombo chenye mfano wa sanduku la agano, ambacho kiliachwa hapo na majeshi ya Ujerumani enzi za ukoloni. Inasemekana kuwa chombo hicho kina miujiza na mambo mengi ya ajabu na kutisha.


Je wewe mdau unasemaje kuhusu chombo hiki cha jabu? Kwa mtazamo wako unadhani kipo wapi? Toa mchango wako kuhusu chombo hiki cha ajabu na kihistoria.

Monday, April 6, 2009

CROP CIRLCES











Some of the world's most interesting phenomenons is the crop circles. Crop circles are areas of cereal or similar crops that have been systematically flattened to form various geometric patterns. The phenomenon itself only entered the public imagination in its current form after the notable appearances in England in the late 1970s. Various scientific and pseudo-scientific explanations were put forward to explain the phenomenon, which soon spread around the world. In 1991, two men, Doug Bower and Dave Chorley, revealed that they had been making crop circles in England since 1978 using planks, rope, hats and wire as their only tools. Circlemakers.org a UK based arts collective founded by John Lundberg have been creating crop circles since the early 1990s. Although the commonly accepted view today is that crop circles are a man-made phenomenon, paranormal explanations, often including UFOs, are still popular.In paranormal circles the study of the crop circle phenomena is called cerealogy. Cerealogists commonly refer to these designs as agriglyphs.

A small portion of the crop circles are made by humans for their own personal reasons. However, the vast majority still prove to be of unknown origin. The scientific community has for the moment deemed the phenomenon of crop circles to be an unexplainable mystery.

Could they be messages from another world? Another galaxy far far away as most alien fanatics think? Could they be signs of the times to come? Could they be just one of mother nature's mysteries? Or are they nothing but hoax?

What is your opinion on them? Tell us what you think they are.

Saturday, April 4, 2009

THE EYE OF GOD - JICHO LA MUNGU


I saw this amazing pic and i wanted to share it with you guys. This is actualy a Nebula that happens to have an appearance of an eye and it being in space or the "heavens", is why it was labelled the "eye of god". Its mind captivating and fascinating.

European astronomers have taken this amazing photo which is actualy a cosmic eye nicknamed the eye of god (jicho la mungu), staring down from space.


The bright blue pupil and the white of the eye are fringed by flesh coloured eyelids. This eye is so big that it's light takes two and a half years to cross from one side to the other. The object is actualy a shell of gas and dust that has been blown off by a faint central star, a fate that our own solar system would come to face five billion years to come. It lies 700 light years away from the constellation of Aquarius and can be dimly seen in small telescopes by amateur astronomers who call it the Helix Nebula. The photo was taken with a giant telescope at the European Southern Observatory, high on the mountain top of La Silla in Chille. It is so detailed that a close-up reveals distant galaxies within the central eyebal.
Drop your comments regarding this amazing pic.

Wednesday, April 1, 2009

SAFINA YA NUHU (NOAH'S ARK) YAPATIKANA





"Safina ya Nuhu imepatikana katika mpaka wa Uturuki na Iran (Turkish-Iranian border) kilometre 32 kutoka mlima Ararat (Mount Ararat)" maneno hayo yalisemwa na kiongozi wa wanasayansi ambao wamekuwa wakifanya utafiti mahala hapo (site of the ark) kwa takribani miaka sita.


Serikali ya Uturuki (Turkish government) ilishawishika na unguduzi huo kiasi kwamba imeitenga sehemu hiyo (site of the ark) ipate kufanyiwa uchunguzi zaidi na imeruhusu uchimbaji wa eneo hilo ambao unatizamiwa kufanyika mwishoni wa mwaka huu wa 2009 ili utafiti wa kina kuhusiana na merikebu hiyo ufanyike.


Sehemu hiyo isiyokuwa na makazi ya watu (site of the ark), ina chombo chenye mfano wa boti au meli kubwa iliyozikwa chini juu juu chini (upside down) resting an altitude of 2,300 metres. Ikiwa na urefu wa mita 170 (170 metres) na upana wa mita 45 (45 metres), chombo hicho kwa vipimo kinalingana na vipimo vya Safina ambayo Mungu alimuagiza Nuhu kutengeza kama kitabu cha Mwanzo 6 (Genesis 6) kwenye Biblia kinavyosema.


Wanasayansi wa Marekani na Mashariki ya Kati wamegundua majiwe makubwa yakiwa na matundu upande wa mwisho wa merikebu hiyo, amabayo yanaaminika kuwa ni "drogue stones" yaliyo kuwa yakitumiwa kuifanya merikebu kuwa stable katika ulimwengu wa nyakati za zamani. Yalikuwa yakifungwa nyuma ya merikebu na kuvutwa.


Salih Bayraktutan, mkubwa wa kitengo cha geology katika chuo kikuu cha Uturuki Ataturk University kwa kupitia vipimo maalum amesema miaka ya chombo inasadikiwa kuwa ni zaidi ya 100,000 (100,000 years).


David fasold mtaalamu wa Kimarekani wa merikebu zilizozama (an American shipwrecked specialist) asiyekuwa na dini (Atheist) ambaye amekuwa akiongoza uchunguzi huo alisema "picha za radar zilizopiga maeneo hayo (site of the ark) zimetokea vizuri sana"


Lkini uchunguzi huo umewakwaza wakristo wengi ambao wamekuwa wakienda nchini Uturuki kutafuta mahala ambapo Safina hiyo ilipoishia wakiamini kuwa inapaswa kupatikana mlima Ararat (Mount Ararat).


Kuna ambao wanaamini kuwa chombo hicho ni Safina ya Nuhu iliyozungumziwa kwenye Biblia na Quran na wengine wanapinga kabisa kuwa siyo kila mtu kwa maoni yake kutokana na uelewa wake. Je wewe wasema nini kuhusiana na ufumbuzi huu? Je ni kweli unaamini kuwa Safina ya Nuhu imepatikana?


Mdau toa maoni yako kuhusiana na chombo hicho cha ajabu kilichogungulika huko mpakani mwa nchi ya Uturuki na Iran.


Tuesday, March 31, 2009

MAUZAUZA




Underwarter camera iliyokuwa imetegeshwa na watafiti wa mambo ya mimea iotayo ndani na kandokando ya maji (swamps), ilikuwa ikipiga picha za mfululizo kila baada ya daika tano. Picha hizo zilipokuja kufanyiwa utafiti, picha moja ambayo ndio hii unayoiona hapa ilitoka ikiwa ina image ya kitu mfano wa binadamu wa ajabu aliyevalia nguo nyeupe. Picha hiyo iliwashangaza sana waliyoiona na wameiweka kwenye frame maalum kama kumbukumbu. Je kwa maoni yako unadhani ni kitu gani hiki kilichopigwa picha? Toa maoni yako mdau kuhusiana na picha hii.

Monday, March 30, 2009

HUYU NI MALAIKA?


Picha hii ilichukuliwa na mwanamke mmoja kwenye state ya Colorado, U.S.A. Ilipigwa wakati wa mashindano ya kupiga picha nyota ambayo walishiriki watu wapatao 150. Mwanamke huyo alitumia camera maalum iliyo na uwezo mkubwa wa kuona mbali kwenye anga na akapiga picha nyota za anga. Bila kugundua ni kitu gani alichokipiga kwenye picha yake akaipeleka picha yake kwa developer. Developer alipoiona akamuuliza alipigaje hiyo picha na akamuuliza kama hajaona kitu chochote cha ajabu kwenye picha hiyo. Kwenye hiyo picha kimeonekana kitu kama kiumbe mfano wa malaika. Ukitazama vizuri utaona mabawa makubwa, kichwa na sura kama ya mwanamke akiwa amevaa taji (crown) la dhahabu likiwa limezungukwa na vito vya thamani, uso wake umegeuka upande, ukiangalia vizuri unaweza kuona sehemu ya jicho, pua, sikio na mdomo. Ukija chini utaona bega la kulia pamoja na mkono ambao sehemu kubwa yake umefunikwa na nyota. Wadau leteni maoni yenu hiki ni kitu gani? Je huyu mwanamke alimpiga picha malaika bila kujua? au pepo (jini)?. Nigependa kupata maoni yako kuhusiana na picha hii.

SAMAKI MTU


Wadau huyu samaki wa ajabu alionekana akiwa amekufa kule Malaysia baada ya tsunami. Mwangalie samaki huyu kwa makini utaona kuwa ana mbavu, mikono na kichwa kama binadamu. Je huyu ni samaki mtu(mermaid)?. Wadau toeni maoni yenu kuhusu kiumbe hiki cha ajabu.